Simba SC imeendelea kuweka hai matumaini yake ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo uliopigwa Uwanja wa KMC Complex.
Mchezo huo ulikuwa na ushindani mkubwa huku timu zote zikihitaji matokeo chanya, lakini ni Simba walioweza kutumia vyema nafasi zao na kuondoka na alama zote tatu muhimu.





