Local,Normal News,Yanga, Azam

Ligi Kuu; Yanga vs Azam Fc kupigwa New Amaan Complex

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Jun 2026
Ligi Kuu; Yanga vs Azam Fc kupigwa New Amaan Complex

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga SC, Ali Kamwe, amethibitisha rasmi kuwa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga dhidi ya Azam FC uliopangwa kupigwa Juni 24 sasa utachezwa katika uwanja wa New Amaan Complex uliopo visiwani Zanzibar.

Yanga SC watakuwa wenyeji wa mchezo huo muhimu ambao una uzito mkubwa katika harakati zao za kutetea ubingwa wa ligi msimu huu.Β 

Ali Kamwe amesema kuwa Yanga tayari imekwishawaarifu rasmi Bodi ya Ligi kuhusu uamuzi wa kubadilisha uwanja na kuhamishia mchezo huo Zanzibar. Uamuzi huo unaonekana kuwa sehemu ya mipango ya kiufundi Yanga ikihitaji kushinda.

Kamwe pia alieleza kuwa baada ya mchezo wa nusu fainali wa Kombe la CRDB Bank Cup dhidi ya Azam FC utakaopigwa Juni 21 katika uwanja wa CCM Kirumba, kikosi cha Yanga kitaelekea visiwani Zanzibar moja kwa moja kujiandaa kwa mtanange hu.

Mchezo huo wa ligi kati ya Yanga na Azam FC umepangwa kupigwa saa 10 jioni, na unatarajiwa kuwa mmoja kati ya mechi zenye ushindani mkali zaidi katika msimu huu wa Ligi Kuu.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
10m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
39m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’