International,Normal News,World Cup, Spain, Cape Verde, Local

Cape Verde yaweka rekodi mechi ya Kwanza Kombe la Dunia ikitoshana nguvu na Hispania

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Jun 2026
Cape Verde yaweka rekodi mechi ya Kwanza Kombe la Dunia ikitoshana nguvu na Hispania

Timu ya taifa ya Cape Verde imeandika historia katika Kombe la Dunia 2026 baada ya kuizuia Hispania kwa sare ya bila kufungana (0-0) kwenye mechi ya ufunguzi ya Kundi H. Matokeo hayo yameifanya Cape Verde kuokota alama yake ya kwanza kabisa katika historia ya mashindano hayo huku ikiweka rekodi katika mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia.

Cape Verde, ambayo inashiriki Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza katika historia yake, ilionyesha nidhamu kubwa ya kiulinzi dhidi ya moja ya timu zinazopewa nafasi ya kutwaa ubingwa. Licha ya Hispania kumiliki mpira kwa muda mrefu na kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga, safu ya ulinzi ya Cape Verde pamoja na kipa mkongwe Vozinha waliweza kuhimili mashambulizi yote na kuhakikisha timu yao inaondoka na pointi muhimu.

Kipa Vozinha mwenye umri wa miaka 40 alikuwa nyota mchezo huo. Ameandika historia pia kwa kuwa mmoja wa wachezaji wenye umri mkubwa zaidi kucheza mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia. Uchezaji wake bora uliwavutia mashabiki wengi akipata umaarufu mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.

Kocha wa Cape Verde, Pedro "Bubista" Brito, alisema kabla ya mchezo kwamba timu yake haikuja Kombe la Dunia kwa ajili ya kushiriki tu bali kushindana. Kauli hiyo ilidhihirika uwanjani baada ya wachezaji wake kuonyesha moyo wa kupambana dhidi ya mabingwa wa Ulaya.

Matokeo hayo yanaifanya Cape Verde kupata alama moja muhimu katika Kundi H, ambalo pia lina timu za Uruguay na Saudi Arabia. Sare hiyo imeipa Cape Verde matumaini ya kuendelea kupambana kwa nafasi ya kufuzu hatua inayofuata katika mashindano hayo.

Kwa upande wa Hispania, sare hiyo imeonekana kama matokeo ya kushtua kwa mashabiki wake kwani ni mechi ambayo walitarajia kuibuka na ushhindi mnono.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
36m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’