Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th June 2026


Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo

Mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi tatu za kuhitimisha raundi ya 27 zinatarajiwa kupigwa.

Mabingwa watetezi Yanga watakuwa na shughuli pevu mbele ya Fountain Gate katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

Ili kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi Yanga inahitaji ushindi au hata matokeo ya sare. Hata hivyo sare inaweza kuwaongezea presha zaidi kufikia malengo yao ya kutetea ubingwa hasa kwa kuzingatia watakuwa na mechi nyingine tatu ngumu dhidi ya Azam Fc, TRA United na JKT Tanzania.

Ushindi wa bao 1-0 ambao watani zao Simba waliupata dhidi ya Mbeya City umewaweka kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama moja baada y kufikisha alama 64.

Hata hivyo Wananchi wasitarajie mtaremko kutoka kwa Fountain Gate kwani nao wanazihitaji alama tatu ili kujiondoa kwenye presha ya kucheza play-off au kushuka daraja.

Pamba Jiji itachuana na Mtibwa Sugar katika mchezo mwingine utakaopigwa saa 10 jioni huku JKT Tanzania wakiikaribisha Tanzania Prisons katika mtanange ambao pia utapigwa saa 10.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.