Local,Transfer News,Tetesi, Simba

Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Jun 2026
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya

Klabu ya Simba SC imeanza harakati za kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao kwa kuonyesha nia ya kumsajili mlinda lango wa Zimbabwe, Nelson Chadya, ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Scottland FC ya nchini humo.

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba zinaeleza kuwa maboresho makubwa yanatarajiwa kufanyika katika eneo la makipa, huku hatma ya makipa waliopo kwa sasa ikibaki kuwa ya kusubiri. Djibrilla Kassali, Moussa Camara na Hussein Abel wote mikataba yao inakaribia kumalizika, hali inayolazimisha klabu hiyo kuanza kutafuta mbadala mapema.

Inaelezwa kuwa Simba inaweza kusajili makipa wawili katika dirisha lijalo la usajili, mmoja akiwa mchezaji wa kigeni na mwingine wa ndani, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha ushindani katika kikosi hicho.

Chadya amekuwa katika kiwango bora msimu huu akiwa na Scottland FC. Katika mechi 20 alizocheza, amefanikiwa kutunza nyavu zake bila kufungwa mabao katika michezo 14, rekodi iliyochangia timu yake kuendelea kushikilia nafasi ya juu kwenye Ligi Kuu ya Zimbabwe.

Chanzo kutoka ndani ya klabu hiyo kilieleza kuwa mchakato wa kutafuta kipa mpya bado unaendelea na hakuna makubaliano yaliyofikiwa kwa mchezaji yeyote hadi sasa.

"Tunaendelea na mchakato wa kutafuta kipa mwingine. Tumetafakari sana na tunaona kuna haja ya kuongeza kipa mwingine. Bado tuko kwenye mazungumzo na mpaka sasa hakuna aliyesajiliwa," kilieleza chanzo hicho.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’