International,Normal News,World Cup, England, Bayern, Tottenham, Local

Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Jun 2026
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia

Nahodha wa timu ya taifa ya England, Harry Kane, ameandika historia mpya katika mashindano ya Kombe la Dunia baada ya kufikisha jumla ya mabao 10, hatua ambayo inamfanya alingane na rekodi ya gwiji wa zamani wa England, Gary Lineker.

Kane alifikia idadi hiyo ya mabao kufuatia mabao yake mawili katika mechi dhidi ya Croatia akiiongoza Uingereza kuanza vyema kampeni ya kulisaka kombe la Dunia kwa ushindi wa mabao 4-2.

Hatua hiyo imeweka jina lake sambamba na Lineker ambaye alifunga mabao 10 katika historia yake ya michuano ya Kombe la Dunia akiwa na Three Lions.

Rekodi hiyo ya Lineker imedumu kwa zaidi ya miongo mitatu, huku akijulikana sana kwa umahiri wake mbele ya lango hasa katika Kombe la Dunia la 1986 na 1990.

Kwa upande wake, Kane ameendelea kuthibitisha ubora wake kama mmoja wa washambuliaji tegemeo wa England katika kizazi cha sasa, akichangia mabao katika mashindano kadhaa ya Kombe la Dunia na kuongeza thamani yake katika historia ya timu hiyo.

Mashabiki wa soka wa England sasa wanasubiri kuona Kane akivunja rekodi hiyo na kujiweka peke yake kileleni kama mfungaji bora wa England katika historia ya Kombe la Dunia.

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’