Klabu ya Azam FC imethibitisha rasmi kumuongezea mkataba kiungo wake mkongwe, Hemed Mao Mkami, ambaye ataendelea kubaki katika kikosi hicho hadi mwaka 2027.
Nyota huyo amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja ambao unaongeza muda wake wa kuitumikia klabu hiyo ya Chamazi, hatua inayoonesha imani kubwa ya benchi la ufundi na uongozi wa Azam FC kwa mchango wake ndani ya timu.





