Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th June 2026


Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Pacome Zouzoua, ameweka wazi kuwa amekumbana na changamoto kubwa ya majeraha msimu huu, hali iliyomlazimu kucheza baadhi ya mechi akiwa na maumivu makali ya goti.

Nyota huyo, anayejulikana kwa uwezo wake mkubwa wa kutengeneza na kufunga mabao, amesema kipindi hicho kilikuwa kigumu kwake, lakini sasa ameimarika na yuko tayari kuisaidia Yanga katika mechi zilizosalia kabla ya kufungwa kwa msimu.

Pacome alionyesha kurejea katika kiwango chake bora baada ya kufunga bao la kwanza la Yanga kwenye ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Fountain Gate. Bao hilo lilikuwa muhimu kwake binafsi na kwa timu katika harakati za kutimiza malengo ya msimu.

Baada ya kufunga, Pacome alionyesha ishara maalumu ya shukrani kuelekea kwa mashabiki wa Yanga, akieleza kuwa ilikuwa ni njia yake ya kuwashukuru kwa sapoti waliompa katika kipindi chote alichokuwa akipambana na majeraha.

β€œIshara ile ni kuwashukuru mashabiki wa Yanga ambao wameweza kunivumilia katika kipindi kigumu. Nilicheza nikiwa na maumivu kwenye goti kwa kipindi kirefu kidogo lakini mara zote wamekuwa pamoja na mimi hata ninapokuwa katika nyakati ngumu uwanjani,” alisema Pacome.

Aliongeza kuwa bao alilofunga dhidi ya Fountain Gate lina maana kubwa kwake katika hatua hii muhimu ya mwisho wa msimu.

β€œGoli dhidi ya Fountain Gate ni muhimu sana kwangu katika wakati huu tunapoelekea mwisho wa msimu. Najiskia vizuri sasa na niko tayari kuwapa mashabiki wetu kile wanachokitarajia kutoka kwetu. Waje kwa wingi uwanjani kutusapoti kwenye mechi hizi za mwisho,” aliongeza.


  

More Stories

Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba
Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba
Today, READ MORE β†’
Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi
Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi
Today, READ MORE β†’
Himid aongeza mwaka Azam Fc
Himid aongeza mwaka Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Today, READ MORE β†’
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Wikiendi ya kusaka wanafainali CRDB Cup
Ni Wikiendi ya kusaka wanafainali CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ratiba ya Ligi Kuu ya Premia 2026/27 hadharani
Ratiba ya Ligi Kuu ya Premia 2026/27 hadharani
Today, READ MORE β†’
Ni kweli Real Madrid ilimtaka Alvarez?
Ni kweli Real Madrid ilimtaka Alvarez?
Today, READ MORE β†’
Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026
Canada yaichapa Qatar 6-0, yaandika historia Kombe la Dunia 2026
Today, READ MORE β†’
Foutain Gate 0-2 Yanga, Ligi Kuu
Foutain Gate 0-2 Yanga, Ligi Kuu
Today, READ MORE β†’