Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th June 2026


Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba

Licha ya kukosa sehemu kubwa ya msimu kutokana na majeraha, kiwango bora alichokionyesha golikipa Moussa Camara kabla ya kuumia kinaendelea kuwa kipimo kwa makipa wa Simba SC, hususan Djibrilla Kassali ambaye amebeba jukumu la kulinda lango la timu hiyo kwa kipindi kirefu cha msimu.

Akizungumza kuelekea fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank pamoja na mwisho wa msimu wa Ligi Kuu ya NBC, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema ubora aliouonesha Camara uliacha alama kubwa ndani ya kikosi hicho.

Ahmed Ally alieleza kuwa mashabiki na wadau wengi wa soka wamekuwa wakilinganisha kiwango cha makipa wa sasa na kile alichokionesha Camara kabla ya kuumia, jambo linaloonesha namna alivyokuwa muhimu ndani ya timu.

"Camara aliweka kiwango kikubwa sana kabla ya kuumia, ndiyo maana hata sasa watu bado wanakitaja na kukilinganisha na makipa waliopo. Hilo linaonesha ubora wake na mchango wake kwa timu," alisema Ahmed Ally.

Kwa sasa Simba inaendelea kujiandaa na michezo muhimu ya mwisho wa msimu huku ikitarajia kumaliza kampeni zake kwa mafanikio katika mashindano ya ndani.


  

More Stories

Nyota Paraguay amekula umeme kwa kuziba mdomo
Nyota Paraguay amekula umeme kwa kuziba mdomo
Today, READ MORE β†’
Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba
Kivuli cha Camara kinavyomtesa Kassali Simba
Today, READ MORE β†’
Brazil yatinga kileleni kundi C baada ya kuichapa Haiti 3-0
Brazil yatinga kileleni kundi C baada ya kuichapa Haiti 3-0
Today, READ MORE β†’
Morocco yaizamisha Scotland, yabeba matumaini ya Afrika
Morocco yaizamisha Scotland, yabeba matumaini ya Afrika
Today, READ MORE β†’
Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba
Mutale na Simba wafikia makubaliano ya kuvunja mkataba
Today, READ MORE β†’
Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi
Pacome afunguka changamoto ya majeraha, atoa ahadi kwa Wananchi
Today, READ MORE β†’
Himid aongeza mwaka Azam Fc
Himid aongeza mwaka Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Kone kuuguza majeraha kwa miezi 6
Today, READ MORE β†’
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Makocha Simba, Coastal Union wafunguka maandalizi nusu fainali CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Wikiendi ya kusaka wanafainali CRDB Cup
Ni Wikiendi ya kusaka wanafainali CRDB Cup
Today, READ MORE β†’