Nyota wa Miguel Almirón ameandika historia ya aina yake katika mashindano ya Kombe la Dunia baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kutokana na kitendo cha kuzungumza na mchezaji wa timu pinzani huku akiziba mdomo, katika mchezo uliowakutanisha Paraguay na Turkey.
Tukio hilo limetokana na utekelezaji wa kanuni mpya za nidhamu zilizotangazwa na FIFA kabla ya kuanza kwa mashindano hayo, ambazo zinazuia mchezaji kuzungumza na mpinzani kwa kuficha mdomo, huku adhabu yake ikiwa ni kadi nyekundu ya moja kwa moja. Mwamuzi alitekeleza sheria hiyo baada ya Almirón kuonekana akimjibu mpinzani wake kufuatia rafu, akiwa ameziba mdomo, jambo lililotafsiriwa kama ukiukwaji wa moja kwa moja wa kanuni hizo mpya.
Licha ya Paraguay kupoteza mchezaji huyo muhimu uwanjani, iliendelea kucheza kwa nidhamu na hatimaye kufanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Uturuki, matokeo yaliyowapa nafasi muhimu ya kujiimarisha katika Kundi D la mashindano hayo.
Kwa upande wa Uturuki, kipigo hicho kimeongeza changamoto kubwa baada ya kupoteza mchezo wake wa pili mfululizo, na sasa inashika nafasi ya mwisho katika kundi ikiwa haina pointi yoyote. Timu hiyo imebakiwa na mchezo mmoja wa mwisho kujaribu kubaki kwenye mashindano.
Msimamo wa Kundi D unaonyesha Marekani ikiwa inaongoza kwa pointi sita, ikifuatiwa na Australia na Paraguay zikiwa na pointi tatu kila moja, huku Uturuki ikiwa mkiani. Kila timu imebakiwa na mchezo mmoja



