Makocha wa Yanga na Azam FC wameonyesha kujiamini huku wakitambiana kuelekea mchezo wa nusu fainali ya Kombe la CRDB unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Kocha wa Yanga, Abdihamid Moalin, amesema ni heshima kubwa kwa klabu hiyo kufanikiwa kucheza hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo, huku akisisitiza kuwa lengo lao kuu ni kushinda mchezo huo na kutinga fainali.





