Hilo ndilo swali kubwa linalozungumzwa na mashabiki wa Yanga kuelekea mchezo muhimu dhidi ya Azam FC katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Baada ya Azam kuichapa Yanga SC kwaΒ mabao 3-2 kwenye nusu fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank, wengi ndani ya kambi ya Wananchi wameanza kujiuliza kama wapinzani wao wanastahili kupewa heshima zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.
Azam wameonyesha kuwa si timu ya kubeza tena, wakijivunia kikosi kipana na kocha Florent Ibenge ambaye anaingia uwanjani bila presha kubwa.
Kwa upande wa Yanga, matumaini makubwa yamebaki kwa nyota kama Maxi Nzengeli, Pacome, Abuya na Okello kuhakikisha historia ya mchezo uliopita haijirudii. Sasa macho yote yataelekezwa New Amaan Complex kuona kama Yanga watachukua tahadhari zaidi dhidi ya Azam au wataingia kwa nguvu wakiamini ubora wao unaweza kuamua mchezo.
Swali linasalia palepale; je, Azam wanapaswa kupewa heshima yao au Yanga wawachukulie kama wapinzani wa kawaida?



