Afrika Kusini imeandika historia mpya katika soka la dunia baada ya kufuzu kwa mara ya kwanza hatua ya mtoano ya Kombe la Dunia kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Korea Kusini usiku wa Juni 24, 2026. Ushindi huo uliifanya Bafana Bafana kumaliza nafasi ya pili katika Kundi A kwa pointi nne na kufuzu hatua ya 32 bora, ambapo sasa itakutana na Canada Juni 28 jijini Los Angeles.





