Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, amesema kikosi chake kinatarajia mchezo wa ushindani dhidi ya Singida BS utakaochezwa kesho, akisisitiza kuwa lengo kuu ni kutumia nafasi zitakazopatikana na kuondoka na alama tatu. Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya mchezo huo, Backer amesema anaiheshimu Singida BS na anaamini haitakuwa mechi rahisi.





