Picha zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zimemweka Rais wa FIFA, Gianni Infantino, kwenye mjadala baada ya kuonekana akiwa katika viwanja viwili tofauti vya Kombe la Dunia 2026 kwa muda unaodaiwa kufanana. Picha moja ilimuonyesha akiwa NRG Stadium mjini Houston wakati wa mchezo wa Ujerumani, huku nyingine ikimuonyesha Lincoln Financial Field mjini Philadelphia kwenye mchezo ambao Ivory Coast iliifunga CuraΓ§ao bao 1-0, jambo lililozua utani na maswali kutokana na umbali wa zaidi ya kilomita 2,000 kati ya miji hiyo.
Ingawa hakuna uthibitisho kwamba Infantino alikuwa viwanja vyote viwili kwa wakati mmoja, picha hizo zimeendelea kuzua mijadala kuhusu ratiba ya viongozi wa FIFA na namna picha zinavyoweza kupotosha muktadha kwenye mitandao ya kijamii.
Wewe unaamini ni mkanganyiko wa muda wa picha ?mbinu ya mawasiliano ya FIFA ? Au una maelezo mengine kuhusu tukio hili?



