Chelsea waendelea kumuwinda Granit Xhaka, Kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media β€’ 29th June 2026


Chelsea waendelea kumuwinda Granit Xhaka, Kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao

Chelsea na Sunderland wanatarajiwa kuendelea na mazungumzo mapya leo kuhusu uwezekano wa kumsajili kiungo wa Uswisi, Granit Xhaka, huku viongozi wakuu wa klabu zote mbili wakiendelea kuwa kwenye mawasiliano ya moja kwa moja. Ingawa dili hilo linaelezwa kuwa gumu, bado halijafikia hatua ya kuvunjika.

Kwa mujibu wa taarifa zinazoendelea kutoka Ulaya, Xhaka ameonyesha nia kubwa ya kurejea London na kufanya kazi tena chini ya kocha Xabi Alonso, ambaye anatajwa kuwa na mpango wa kumjumuisha katika kikosi chake cha Chelsea kwa ajili ya msimu mpya.

Inaelezwa kuwa kiungo huyo yuko tayari kukubali masharti yoyote ya mkataba ili kuhakikisha anatimiza ndoto ya kurejea Stamford Bridge na kuanza ukurasa mpya wa kazi yake chini ya Alonso.

Chelsea wanaamini uzoefu, uongozi na ubora wa Xhaka katikati ya uwanja unaweza kuwa nyongeza muhimu katika mradi mpya wa klabu hiyo, huku Alonso akimtazama kama mmoja wa wachezaji wanaoweza kuipa timu utulivu na ushindani mkubwa.

Hata hivyo, makubaliano rasmi bado hayajafikiwa, na pande zote zinaendelea kujadili masuala ya mwisho ya uhamisho huo. Ikiwa mazungumzo ya leo yatazaa matunda, Xhaka anaweza kuwa mmoja wa usajili wa kushtukiza wa Chelsea katika dirisha hili la majira ya joto.


  

More Stories

Moalin - Tunahitaji Ushindi Tuwe Mabingwa
Moalin - Tunahitaji Ushindi Tuwe Mabingwa
Today, READ MORE β†’
Mechi tatu kupigwa leo ndani ya kombe la dunia 2026, Hatua ya 32 Bora.
Mechi tatu kupigwa leo ndani ya kombe la dunia 2026, Hatua ya 32 Bora.
Today, READ MORE β†’
Moallin au Steve Barker, dakika 90 za mwisho za kuandika historia ya ubingwa
Moallin au Steve Barker, dakika 90 za mwisho za kuandika historia ya ubingwa
Today, READ MORE β†’
Chelsea waendelea kumuwinda Granit Xhaka, Kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao
Chelsea waendelea kumuwinda Granit Xhaka, Kuimarisha kikosi chao kuelekea msimu ujao
Today, READ MORE β†’
Pamba Jiji Yakabiliwa Na Hatari Ya Kuporomoka Kikosi, Nyota Wake Wahusishwa Na Timu Mbalimbali
Pamba Jiji Yakabiliwa Na Hatari Ya Kuporomoka Kikosi, Nyota Wake Wahusishwa Na Timu Mbalimbali
Today, READ MORE β†’
JKT Tanzania : Tunatafuna mfupa uliowashinda
JKT Tanzania : Tunatafuna mfupa uliowashinda
Today, READ MORE β†’
Kinda Afrika kusini Aiteka WC2026, Atabiliwa Makubwa
Kinda Afrika kusini Aiteka WC2026, Atabiliwa Makubwa
Today, READ MORE β†’
Hatma ya Fountain Gate, Mbeya City, Mtibwa na Tanzania Prison Kufahamika kesho
Hatma ya Fountain Gate, Mbeya City, Mtibwa na Tanzania Prison Kufahamika kesho
Today, READ MORE β†’
Canada waiondoa Bafana bafana dakika za jioni, Watinga 16 bora kwa mara ya kwanza
Canada waiondoa Bafana bafana dakika za jioni, Watinga 16 bora kwa mara ya kwanza
Today, READ MORE β†’
Afrika Kusini na Canada kufungua 32 bora leo
Afrika Kusini na Canada kufungua 32 bora leo
Today, READ MORE β†’