Taharuki Yazuka kabla ya kuelekea kwenye Mchezo wa mtoano kati ya Mexico dhidi ya Ecuardo.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media β€’ 30th June 2026


Taharuki Yazuka kabla ya kuelekea kwenye Mchezo wa mtoano kati ya Mexico dhidi ya Ecuardo.

Kumeibuka taharuki kuelekea mchezo muhimu wa hatua ya 32 bora ya Kombe la Dunia 2026 kati ya Mexico na Ecuador, baada ya mamia ya mashabiki wa Mexico kukusanyika nje ya hoteli inayofikia timu ya taifa ya Ecuador wakipiga honi za magari, tarumbeta, spika na kuimba nyimbo usiku kucha.

Taarifa zinaeleza kuwa baadhi ya wachezaji wa Ecuador walionekana wakichungulia madirishani kuona kilichokuwa kikiendelea, huku mashabiki hao wakidaiwa kupanga kuendelea na kelele hizo usiku mzima kwa lengo la kuwanyima wapinzani wao usingizi kabla ya mchezo huo muhimu.

Hatua hiyo imezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki wa soka duniani, ambapo baadhi wanaiona kama mbinu ya kuwapa Mexico faida ya nyumbani, huku wengine wakisema inakiuka misingi ya mchezo wa haki (fair play) na heshima kwa wapinzani.

Mexico na Ecuador zinakutana saa 4:00 usiku (EAT) wa kuamkia kesho mjini Mexico City, katika pambano ambalo mshindi atafuzu hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia 2026. Macho ya dunia sasa yataelekezwa uwanjani kuona kama kelele hizo zitakuwa na athari yoyote kwa maandalizi ya Ecuador au kama watajibu kwa matokeo ndani ya dakika 90.


  

More Stories

Arsenal Sio Mabingwa Kama Lile Sio Goli : Klopp
Arsenal Sio Mabingwa Kama Lile Sio Goli : Klopp
Today, READ MORE β†’
Wababe wa Yanga Kuzindua Jezi za Msimu Ujao Leo
Wababe wa Yanga Kuzindua Jezi za Msimu Ujao Leo
Today, READ MORE β†’
Taharuki Yazuka kabla ya kuelekea kwenye Mchezo wa mtoano kati ya Mexico dhidi ya Ecuardo.
Taharuki Yazuka kabla ya kuelekea kwenye Mchezo wa mtoano kati ya Mexico dhidi ya Ecuardo.
Today, READ MORE β†’
Nani Kuondoka na Kiatu cha Dhahabu NBC ?
Nani Kuondoka na Kiatu cha Dhahabu NBC ?
Today, READ MORE β†’
Morocco waing\'oa Uholanzi na kufuzu 16 bora
Morocco waing\'oa Uholanzi na kufuzu 16 bora
Today, READ MORE β†’
Paraguay Yatamatisha Safari ya Ujerumani WC2026, Vilio vya Tawala
Paraguay Yatamatisha Safari ya Ujerumani WC2026, Vilio vya Tawala
Today, READ MORE β†’
Hatuna Mpango na Fadlu : Ally Kamwe
Hatuna Mpango na Fadlu : Ally Kamwe
Today, READ MORE β†’
Brazil wapindua meza kibabe, Na kuiondoa Japan kombe la dunia 2026
Brazil wapindua meza kibabe, Na kuiondoa Japan kombe la dunia 2026
Today, READ MORE β†’
Kocha wa zamani Yanga aibukia Tunisia
Kocha wa zamani Yanga aibukia Tunisia
Today, READ MORE β†’
Fei Toto, Mossi, Okello watatoana damu ufungaji bora
Fei Toto, Mossi, Okello watatoana damu ufungaji bora
Today, READ MORE β†’