Manchester City wanaendelea kuonyesha nia yao ya kuwekeza kwa vipaji vya muda mrefu baada ya kuibuka na taarifa kwamba klabu hiyo inafikiria kufanya uhamisho wa kiungo kinda wa Morocco, Ayyoub Bouaddi, kuanzia majira ya joto ya mwaka 2027.
Kinda huyo anayechukuliwa kama mmoja wa vipaji vinavyongβaa zaidi baada ya kufanya vyema kwenye kikosi cha Morocco kwenye michuano ya kombe la Dunia, ameweka macho ya mabosi wa City.
City wafanya mawasiliano ya awali
Taarifa zinaeleza kuwa Manchester City tayari wamefanya mawasiliano ya awali na upande wa mchezaji huyo, huku wakijua wazi kwamba ushindani wa kumsajili ni mkali kutokana na vilabu vingi vya Premier League pia kumfuatilia kwa karibu.
Hata hivyo, Lille bado wanashikilia msimamo mkali kuhusu mustakabali wa nyota huyo, wakionekana kuwa na mpango wa kumhifadhi kwa angalau msimu mmoja zaidi kabla ya kuanza mazungumzo makubwa ya uhamisho.
Bei ya kuvunja benki
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, Lille wanamthamini Bouaddi kwa kiasi kikubwa, wakianza mazungumzo ya bei kuanzia euro milioni 75 hadi 80 pamoja na nyongeza (add-ons), kiwango kinachoonyesha jinsi klabu hiyo inavyomchukulia kama mchezaji wa thamani ya juu sana ya baadaye.
Vita vya usajili barani Ulaya
Mbali na Manchester City, klabu kadhaa kubwa za Premier League pia zinaonyesha nia ya kumsajili kiungo huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi mbalimbali katikati ya uwanja. Hali hii inafanya vita vya usajili wake kuwa wazi na vinavyoweza kuwa vya ushindani mkubwa zaidi kwenye dirisha hili.
Kwa umri wake mdogo na uwezo anaouonyesha, Ayyoub Bouaddi anaonekana kuwa mmoja wa vipaji vinavyoweza kuunda kizazi kipya cha viungo wa kisasa barani Ulaya. Ikiwa Manchester City watafanikiwa kumvutia, basi itakuwa hatua nyingine ya kuimarisha mradi wao wa muda mrefu wa kuendelea kutawala soka la Ulaya.



