Kikosi Cha Azam FC kimeondoka jijini Dar es salaam kuelekea visiwani Zanzibar tayari kwa mchezo wa fainali CRDB Bank Federation dhidi ya Simba , mchezo ambao utafanyika uwanja wa Gombani, Pemba Jumamosi hii .
Ikumbukwe Azam FC wanaingia fainali hii baada ya kuinyoosha Yanga Sc kwa mabao matatu pale katika Dimba la Ccm Kirumba Mwanza huku kwa upande wa Simba wakitinga fainali hiyo baada ya kuwaondoa wagosi wa kaya Coastal Union.

Β



