Rais wa FC Barcelona, Joan Laporta, amethibitisha kwa mara ya kwanza kuwa klabu hiyo ilituma ofa rasmi kwa Atlético Madrid kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Argentina, Julián Álvarez.
Kauli hiyo imeonyesha nia ya Barcelona kuongeza nguvu katika safu yake ya ushambuliaji kwa mmoja wa washambuliaji wanaoonekana kuwa na thamani kubwa kwa sasa.





