Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, amesema lengo lake kwa msimu ujao ni kuona klabu hiyo ikifanya makubwa zaidi kwa kutwaa makombe yote yanayoshindaniwa ndani na nje ya Tanzania.
Barker amesema anatamani paredi ya msimu ujao iwe kubwa zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka huu, jambo litakalowezekana endapo Simba itafanikiwa kushinda mataji yote ya ndani huku ikiweka mkazo mkubwa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Amesisitiza kuwa Simba haitaridhika na mafanikio ya sasa pekee, bali itaendelea kujijenga ili kushindana kwa kiwango cha juu barani Afrika, akieleza kuwa ndoto yake ni kuiletea klabu heshima kubwa zaidi kupitia mafanikio ya kimataifa.



