Zinedine Zidane anatajwa kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Ufaransa baada ya kukamilika kwa safari ya Didier Deschamps kwenye benchi la ufundi la Les Bleus.
Taarifa zinaeleza kuwa makubaliano ya awali kati ya Zidane na Shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF) tayari yalikuwepo kwa muda, huku hatua rasmi zikisubiri kukamilishwa baada ya Kombe la Dunia.





