International,Normal News,WC2026, England, Tuchel, Rice, Messi, Local

Tuchel Aweka Wazi Hatma Yake Baada ya England Kutolewa Kombe la Dunia

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
16 Jul 2026
Tuchel Aweka Wazi Hatma Yake Baada ya England Kutolewa Kombe la Dunia

Kocha wa Timu ya Taifa ya England, Thomas Tuchel, amethibitisha kuwa ataendelea kuinoa timu hiyo hadi fainali za Euro 2028, licha ya England kuondolewa kwenye Kombe la Dunia 2026 baada ya kufungwa mabao 2-1 na Argentina katika mchezo wa nusu fainali uliochezwa jijini Atlanta. England walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Anthony Gordon kabla ya Enzo Fernández na Lautaro Martínez kuigeuzia kibao Argentina.

Tuchel alisema hana mpango wa kuondoka kwenye nafasi hiyo, akisisitiza kuwa ataendelea kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa mkataba wake. Kauli hiyo imeungwa mkono na Shirikisho la Soka la England (FA), ambalo limethibitisha kuwa linaendelea kuwa na imani na kocha huyo kuelekea mashindano ya Euro 2028.

Kocha huyo raia wa Ujerumani alianza kuinoa England Januari 2025 na baadaye akaongeza mkataba wake hadi mwaka 2028, baada ya kuiongoza timu hiyo kufuzu Kombe la Dunia bila kupoteza mchezo hata mmoja katika hatua za kufuzu. Wasaidizi wake Anthony Barry, Henrique Hilário, Nico Mayer na James Melbourne pia wataendelea kuwa sehemu ya benchi la ufundi hadi kipindi hicho.

Licha ya kuungwa mkono na FA, Tuchel amekosolewa na baadhi ya wachambuzi wa soka kutokana na maamuzi yake ya kimbinu katika mchezo dhidi ya Argentina, hususan kubadili mfumo wa timu kwenda mabeki watano baada ya England kupata bao la kuongoza. Hatua hiyo ilitajwa kuwa ilipunguza nguvu ya ushambuliaji na kuipa Argentina nafasi ya kurejea mchezoni.

Baada ya kuondolewa katika mbio za ubingwa, England sasa itaelekeza nguvu zake kwenye mchezo wa kusaka nafasi ya tatu dhidi ya Ufaransa, huku Tuchel akianza maandalizi ya kujenga kikosi kitakachowania ubingwa wa Euro 2028, mashindano yatakayofanyika England, Scotland, Wales na Ireland.

More Stories

Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
9h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE →
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
1d ago
READ MORE →