International,Transfer News,Morgan Rogers, Chelsea, Arsenal, EPL,Transfer Window

Chelsea yaipiga bao Arsenal kwa Morgan Rogers wa Aston Villa, Saa chache zijazo kutangazwa

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
18 Jul 2026
Chelsea yaipiga bao Arsenal kwa Morgan Rogers wa Aston Villa, Saa chache zijazo kutangazwa

Chelsea imekamilisha dili la kumsajili Morgan Rogers kutoka Aston Villa baada ya kufikia makubaliano rasmi kati ya klabu hizo mbili, huku ikiwahi mpango wa Arsenal, ambao ulikuwa ukijiandaa kuwasilisha ofa rasmi kwa nyota huyo.

Kwa mujibu wa taarifa, Chelsea imekubaliwa ofa yenye thamani ya pauni milioni 117 (Β£117m), na hivyo kushinda mbio za kumsajili mmoja wa wachezaji wenye vipaji vikubwa zaidi nchini England.

Makubaliano ya masharti binafsi kati ya Rogers na Chelsea tayari yamekamilika, ambapo nyota huyo atasaini mkataba wa muda mrefu hadi Juni 2032, ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Rogers anatarajiwa kuwasili London siku ya Jumatatu kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kusaini rasmi mkataba wake. Taarifa zinaeleza kuwa nyaraka zote za uhamisho tayari zimekamilika, huku Chelsea ikifanya kazi kwa kasi kubwa ili kufunga dili hilo ndani ya saa 24 na kuizidi Arsenal.

Usajili huo ni sehemu ya mipango ya kocha Xabi Alonso ya kuendelea kujenga kikosi chenye ushindani mkubwa kuelekea msimu mpya. Chelsea imeonyesha dhamira ya kutwaa vipaji bora sokoni kwa kufanya maamuzi ya haraka kabla ya klabu nyingine kuingilia dili.

Iwapo kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa, Morgan Rogers atatangazwa rasmi kama mchezaji mpya wa Chelsea mara baada ya kukamilisha vipimo vya afya na kusaini mkataba wake, katika moja ya usajili mkubwa zaidi wa dirisha hili la majira ya joto

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
3h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
13h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’