Chelsea imekamilisha dili la kumsajili Morgan Rogers kutoka Aston Villa baada ya kufikia makubaliano rasmi kati ya klabu hizo mbili, huku ikiwahi mpango wa Arsenal, ambao ulikuwa ukijiandaa kuwasilisha ofa rasmi kwa nyota huyo.
Kwa mujibu wa taarifa, Chelsea imekubaliwa ofa yenye thamani ya pauni milioni 117 (Β£117m), na hivyo kushinda mbio za kumsajili mmoja wa wachezaji wenye vipaji vikubwa zaidi nchini England.
Makubaliano ya masharti binafsi kati ya Rogers na Chelsea tayari yamekamilika, ambapo nyota huyo atasaini mkataba wa muda mrefu hadi Juni 2032, ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.
Rogers anatarajiwa kuwasili London siku ya Jumatatu kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kusaini rasmi mkataba wake. Taarifa zinaeleza kuwa nyaraka zote za uhamisho tayari zimekamilika, huku Chelsea ikifanya kazi kwa kasi kubwa ili kufunga dili hilo ndani ya saa 24 na kuizidi Arsenal.
Usajili huo ni sehemu ya mipango ya kocha Xabi Alonso ya kuendelea kujenga kikosi chenye ushindani mkubwa kuelekea msimu mpya. Chelsea imeonyesha dhamira ya kutwaa vipaji bora sokoni kwa kufanya maamuzi ya haraka kabla ya klabu nyingine kuingilia dili.
Iwapo kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa, Morgan Rogers atatangazwa rasmi kama mchezaji mpya wa Chelsea mara baada ya kukamilisha vipimo vya afya na kusaini mkataba wake, katika moja ya usajili mkubwa zaidi wa dirisha hili la majira ya joto