Local,Normal News,Simba Sc

Simba Day 2026 kufanyika rasmi Agosti 8 Uwanja wa Uhuru

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Jul 2026
Simba Day 2026 kufanyika rasmi Agosti 8 Uwanja wa Uhuru

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, ametangaza rasmi kuwa tamasha la Simba Day 2026 litafanyika Jumamosi, Agosti 8, 2026 katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, likiwa ni tukio maalum la utambulisho wa kikosi kitakachoitumikia klabu hiyo katika msimu mpya wa mashindano.

Semaji amebainisha kuwa uamuzi wa kuhamishia tamasha hilo kwenye uwanja wa Uhuru umefanyika ili kupisha matengenezo makubwa yanayoendelea kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa kuelekea fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2027)

"Simba Day 2026 itafanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, kutokana na ukubwa wa tamasha hili duniani tunatamani kufanyika kwenye Uwanja wa Mkapa lakini kwa sasa upo kwenye matengenezo hivyo uwanja ambao utatumika ni Uwanja wa Uhuru. Tayari tumefanya ukaguzi na kupokea maelekezo kutoka kwa wasimamizi. Tamasha hilo litatumika pia kuadhimisha miaka 90 ya Simba Sports Club," alisema

Ahmed amesema maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri, huku uongozi wa klabu ukiwa umejipanga kuhakikisha mashabiki wanapata burudani pamoja na fursa ya kushuhudia kwa mara ya kwanza wachezaji wapya waliosajiliwa pamoja na nyota watakaobaki kukipigania kikosi cha Wekundu wa Msimbazi.

Aidha, Simba Day itakuwa sehemu ya kuhamasisha mshikamano kati ya klabu na mashabiki wake kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu, Kombe la Shirikisho pamoja na mashindano ya kimataifa, huku maelfu ya mashabiki wakitarajiwa kujitokeza kuipa sapoti timu yao.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’