Manchester United wapendekeza Rashford abadilishwe na Manu Koné
Manchester United wamewasilisha pendekezo la kubadilishana wachezaji kwa kuhusisha Marcus Rashford na kiungo wa AS Roma, Manu Koné. Hata hivyo, mshahara wa Rashford wa €11 milioni kwa msimu umeendelea kuwa kikwazo kikubwa katika mazungumzo hayo.
Barcelona waingia kwenye mbio za Rodri
Barcelona wameingia rasmi kwenye mbio za kumsajili kiungo wa Manchester City, Rodri, kufuatia jeraha la muda mrefu la Frenkie de Jong. Hata hivyo, Real Madrid na Paris Saint-Germain pia zinaendelea kuwania saini ya nyota huyo wa Hispania..jpg)
Arsenal waongeza kasi kwenye dili la Bruno Guimarães
Arsenal wanatarajiwa kuanzisha mazungumzo mapya na Newcastle United wiki ijayo kuhusu usajili wa kiungo Bruno Guimarães. Makubaliano binafsi na mchezaji tayari yanadaiwa kuwepo, huku ofa ya awali ya £70 milioni ikitarajiwa kuongezwa. Hatma ya dili hilo sasa inategemea msimamo wa Newcastle kuhusu ada ya uhamisho na uamuzi wao wa kumuuza nyota huyo.
Fenerbahçe na Galatasaray wapigania Rafael Leão
Fenerbahçe bado wana nia ya kumsajili winga wa AC Milan, Rafael Leão, huku ujumbe wa klabu hiyo ukitarajiwa kusafiri kwenda Italia wiki hii kwa mazungumzo zaidi. Wakati huohuo, Galatasaray wameweka mezani ofa ya mshahara wa karibu €12 milioni kwa msimu ili kumshawishi nyota huyo..jpg)
Manchester City wamwekea jicho Marc Bernal
Manchester City wamemtaja kiungo chipukizi wa Barcelona, Marc Bernal (19), kama mbadala wa Rodri endapo ataondoka. Chelsea na Arsenal pia wanaendelea kumfuatilia, huku Bernal akiwa na mkataba hadi 2029 na kipengele cha kuachiliwa cha €500 milioni. 
Liverpool wakataa nafasi ya kumsajili Vinícius Jr
Kambi ya Vinícius Jr ilimtoa nyota huyo kwa Liverpool katika dirisha hili la usajili, lakini klabu hiyo haikuonyesha nia ya kuendelea na mazungumzo. Badala yake, Liverpool wameamua kuelekeza nguvu zao katika kusajili winga wa kulia..jpg)
Arsenal, Spurs na Roma wamfuatilia Schjelderup
Arsenal, Tottenham Hotspur na AS Roma zinaonyesha nia ya kumsajili winga wa Benfica, Andreas Schjelderup. Hata hivyo, Benfica hawapo tayari kumuachia kirahisi na wameweka kipengele cha kuachiliwa cha €100 milioni. .jpg)
Juventus waanza mazungumzo ya Zion Suzuki
Juventus wameanza mazungumzo na Parma kwa ajili ya kumsajili kipa Zion Suzuki, huku Emiliano Martínez na Guglielmo Vicario wakiendelea kuwa kwenye orodha ya chaguo. Parma wanahitaji zaidi ya €30 milioni, jambo linalowafanya Juventus kutafuta njia ya kupunguza gharama za usajili huo.