Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said, amesema klabu hiyo bado haijafunga rasmi shughuli za usajili licha ya kufanya maboresho makubwa ya kikosi kuelekea msimu mpya wa mashindano.
Hersi amesema Yanga bado ina mpango wa kuongeza mchezaji mmoja ambaye amemtaja kama “funga kazi”, ambaye anatarajiwa kutambulishwa kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.





