Klabu ya Simba SC ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji wa Afrika Kusini, Neo Maema, kwa mkataba wa mkopo wa msimu mzima kutoka Mamelodi Sundowns.
Kwa mujibu wa taarifa, Mamelodi Sundowns hivi karibuni ilimuongezea Maema mkataba mpya wa miaka miwili kabla ya kufikia uamuzi wa kumtoa tena kwa mkopo ili apate nafasi zaidi ya kucheza.





