Mshambuliaji wa kimataifa wa Angola, Laurindo Dilson Maria Aurélio "Depú", anatarajiwa kuondoka Yanga SC katika dirisha hili la usajili, huku klabu yake ya zamani, Petro de Luanda, ikionyesha nia kubwa ya kumrejesha nyumbani.
Hata hivyo, mazungumzo kati ya Petro de Luanda na Yanga yameripotiwa kusuasua kutokana na kutofikiwa kwa makubaliano ya ada ya uhamisho.





