Nyota wa soka wa Misri, Mohamed Salah, yuko hatua za mwisho kukamilisha uhamisho wake kwenda klabu ya Trabzonspor ya Uturuki baada ya pande zote kuingia katika mazungumzo rasmi ya usajili.
Trabzonspor imethibitisha rasmi kuwa imeanza mazungumzo ya kumshawishi Salah kujiunga na kikosi hicho kama mchezaji huru kufuatia kuondoka kwake Liverpool mwishoni mwa msimu uliopita.





