Kiungo mkongwe na nyota wa zamani wa timu ya taifa 'Taifa Stars', Jonas Gerard Mkude, amerejea rasmi uwanjani baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na klabu ya Mashujaa FC ya mkoani Kigoma.
Mkude anajiunga na maafande hao kama mchezaji huru, akitokea mkoani Dar es Salaam ambapo alikuwa nje ya uwanja kwa msimu mmoja tangu alipoondoka Yanga.





