Serikali: Tamasha la Taifa kuchochea utamaduni, utaifa na uchumi bunifu

Jairo Mtitu By Jairo Mtitu β€’ 24th August 2026


Serikali: Tamasha la Taifa kuchochea utamaduni, utaifa na uchumi bunifu

Serikali imesema Tamasha la Taifa litakuwa nyenzo muhimu katika kulinda, kutunza na kuendeleza utamaduni wa Mtanzania, huku likitumika pia kuimarisha utaifa na mshikamano, kukuza uchumi bunifu, kufungua fursa za ajira na biashara, pamoja na kuitangaza Tanzania kupitia utalii wa kiutamaduni.

Akitoa taarifa kuhusu maandalizi ya tamasha hilo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema tamasha hilo linatarajiwa kufanyika mkoani Morogoro kuanzia Agosti 25 hadi 29, 2026.

Msigwa amesema tamasha hilo litawakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya utamaduni na ubunifu, likiwemo vikundi 28 vya utamaduni, wasanii 30, wajasiriamali 70 pamoja na vijana 5,000.

Amesema uwepo wa makundi hayo unalenga kutoa nafasi kwa washiriki kuonyesha vipaji, bidhaa na kazi zao za ubunifu, huku wananchi wakipata fursa ya kujifunza na kufurahia utajiri wa tamaduni mbalimbali zinazopatikana nchini.

Kwa mujibu wa Msigwa, tamasha hilo pia ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha utamaduni wa Tanzania unatambulika zaidi ndani na nje ya nchi, sambamba na kutumia utamaduni kama chanzo cha fursa za kiuchumi, ajira na biashara kwa wananchi, hasa vijana.

Aidha, ametoa rai kwa wananchi kushiriki kwa wingi katika Tamasha la Taifa ili kupata nafasi ya kushuhudia na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na utamaduni wa Mtanzania, ikiwemo ngoma za asili, vyakula vya asili na mavazi ya asili.

Mbali na burudani na maonesho ya kitamaduni, tamasha hilo pia litakuwa na mdahalo wa kitaifa utakaojikita katika kuwawezesha vijana kushiriki katika kulinda maadili, hatua ambayo Serikali inaamini itasaidia kujenga kizazi kinachothamini utamaduni na misingi ya maadili ya taifa.

Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa utamaduni katika kujenga umoja wa kitaifa na kukuza uchumi, huku Tamasha la Taifa likitarajiwa kuwa moja ya majukwaa yatakayounganisha utamaduni, ubunifu, biashara na utalii kwa manufaa ya Watanzania.


  

More Stories

Mohamed Salah Aanza Vema Trabzonspor
Mohamed Salah Aanza Vema Trabzonspor
Today, READ MORE β†’
Luvanga Atupia Bao Saba Katika Ushindi wa Al Nassr
Luvanga Atupia Bao Saba Katika Ushindi wa Al Nassr
Today, READ MORE β†’
Serikali: Tamasha la Taifa kuchochea utamaduni, utaifa na uchumi bunifu
Serikali: Tamasha la Taifa kuchochea utamaduni, utaifa na uchumi bunifu
Today, READ MORE β†’
Barcelona yaanza kutetea ubingwa La Liga kwa kishindo
Barcelona yaanza kutetea ubingwa La Liga kwa kishindo
Today, READ MORE β†’
Azam Fc, Mbeya City zatakata ligi kuu
Azam Fc, Mbeya City zatakata ligi kuu
Today, READ MORE β†’
EPL Updates, Brighton, City mambo mazuri huku Liverpool ikianza na sare.
EPL Updates, Brighton, City mambo mazuri huku Liverpool ikianza na sare.
Today, READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 2-1 Pamba Jiji
Highlights : Azam Fc 2-1 Pamba Jiji
Today, READ MORE β†’
Bouaddi kurithi mikoba ya Rodri Manchester City
Bouaddi kurithi mikoba ya Rodri Manchester City
Today, READ MORE β†’
Manqoba akiri JKT Tanzania sio ya kubeza
Manqoba akiri JKT Tanzania sio ya kubeza
Today, READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 20, August 23 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 20, August 23 2026
Today, READ MORE β†’