Mshambuliaji wa Tanzania Clara Luvanga ameendelea kung'ara nchini Saudi Arabia baada ya kufunga mabao saba katika ushindi wa 12-0 wa Al Nassr Women dhidi ya FC CSKA Dushanbe, katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Bara la Asia uliochezwa nchini humo.
Luvanga alifunga mabao hayo dakika za 33, 35, 39, 69, 74, 87 na 89, akitoa mchango mkubwa katika ushindi huo mnono wa Al Nassr. Mabao hayo yameendelea kuonyesha uwezo wake wa kufunga na kumfanya kuwa miongoni mwa wachezaji wanaofanya vizuri katika mashindano hayo.
Kwa jumla, Luvanga sasa amefikisha mabao 12 katika mashindano hayo baada ya kucheza michezo mitatu, huku akibaki kuwa moja ya nyota muhimu katika safu ya ushambuliaji ya Al Nassr Women.



