LASK, Bodo/Glimt na Sabah Fc zaandika historia UEFA Champions League.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media β€’ 26th August 2026


LASK, Bodo/Glimt na Sabah Fc zaandika historia UEFA Champions League.

Hatua ya mchujo wa UEFA Champions League imeendelea kuandika simulizi za kuvutia, huku LASK ikiwa miongoni mwa timu zilizofanya comeback kubwa zaidi. LASK ilikuwa nyuma kwa jumla ya mabao 4-0 dhidi ya Celtic mapema katika mchezo wa mkondo wa pili, lakini ilifunga mabao manne mfululizo na kulazimisha mchezo kuingia muda wa ziada. Sam Adeniran alifunga bao la ushindi dakika ya 109, na kuipa LASK nafasi ya kufuzu Champions League kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu.

Kwa upande mwingine, Bodø/Glimt ya Norway imerejea tena kwenye hatua ya UEFA Champions League baada ya kuifunga NEC Nijmegen kwa jumla ya mabao 6-1 katika michezo miwili ya mchujo. Bodø/Glimt imeendelea kuonyesha ukuaji mkubwa katika miaka ya hivi karibuni na sasa imefanikiwa kurejea kwenye jukwaa kubwa la soka la klabu barani Ulaya.

Historia nyingine imeandikwa na Sabah FC, ambao wamefuzu kwa mara ya kwanza kabisa katika historia yao kucheza UEFA Champions League. Klabu hiyo, ambayo ilianzishwa miaka minane tu iliyopita, imeweza kufika hatua hii ndani ya kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake, jambo linaloifanya safari yao kuwa moja ya simulizi za kipekee katika mchujo wa msimu huu.

Mchujo wa Champions League umeonyesha wazi kuwa historia na ukubwa wa jina pekee havitoshi uwanjani. LASK imefanya comeback ya dakika za mwisho, Bodø/Glimt imerudi kwenye mashindano na Sabah FC imeandika ukurasa mpya katika historia yake ndani ya miaka minane tu. 


  

More Stories

Matola afunguka maandalizi ya Simba kuikabili Coastal Union
Matola afunguka maandalizi ya Simba kuikabili Coastal Union
Today, READ MORE β†’
Ayyoub Bouaddi atua Manchester City kwa ada ya rekodi
Ayyoub Bouaddi atua Manchester City kwa ada ya rekodi
Today, READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 14, August 26 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 14, August 26 2026
Today, READ MORE β†’
LASK, Bodo/Glimt na Sabah Fc zaandika historia UEFA Champions League.
LASK, Bodo/Glimt na Sabah Fc zaandika historia UEFA Champions League.
Today, READ MORE β†’
Bruno Fernandes Mchezaji Bora wa Mwaka EPL 2025/26 Kwa Kura za Wachezaji
Bruno Fernandes Mchezaji Bora wa Mwaka EPL 2025/26 Kwa Kura za Wachezaji
Today, READ MORE β†’
NBC Premier League: Namungo na Polisi Tanzania Zapata Ushindi.
NBC Premier League: Namungo na Polisi Tanzania Zapata Ushindi.
Today, READ MORE β†’
Xabi Alonso - Enzo Akiondoka Chelsea Sitoshangaa
Xabi Alonso - Enzo Akiondoka Chelsea Sitoshangaa
Yesterday, READ MORE β†’
NBC Premier League Leo: Michezo Miwili Yaendelea
NBC Premier League Leo: Michezo Miwili Yaendelea
Yesterday, READ MORE β†’
Dickson Job na Clement Mzize Kurejea Kikosini Karibuni
Dickson Job na Clement Mzize Kurejea Kikosini Karibuni
Yesterday, READ MORE β†’
Chelsea Yaanza Premier League kwa Ushindi Dhidi ya Fulham.
Chelsea Yaanza Premier League kwa Ushindi Dhidi ya Fulham.
Yesterday, READ MORE β†’