Kiungo mshambuliaji wa yanga Stephen Azizi KI anatarajiwa kuwa sehemu ya wachezaji wa yanga ambao watawakilisha Timu hiyo katika mchezo wa raundi ya tano ya NBC hii Leo dhidi ya Fountain Gate
Taarifa hiyo inakuja kufuatia maneno ya Kocha Mkuu wa Timu hiyo Manqoba Mngqithi alipozungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa pamba jiji wiki iliyopita kuwa nyota huyo atakuwa tayari kabla ya mechi za Kimataifa.
Yanga inashuka uwanjani hii leo majira ya saa 10 jioni katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kisha kurejea tena uwanjani Septemba 5 kwenye mchezo wa kwanza Kimataifa dhidi ya Gaborone united ya Botswana



