Mabula aibukia JS Kabylie

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st September 2026


Mabula aibukia JS Kabylie

Kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Alphonce Mabula Msanga, hatimaye ameibukia katika klabu ya JS Kabylie ya Algeria, baada ya kuhusishwa kwa nguvu na mabingwa wa Tanzania, Yanga SC, katika dirisha lililopita la usajili.

Mabula, mwenye umri wa miaka 23, amejiunga na JS Kabylie kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Shamaxi FK ya Azerbaijan mwishoni mwa Juni 2026.

Taarifa kutoka Algeria zinaeleza kuwa amesaini mkataba wa miaka mitatu na klabu hiyo ya Tizi Ouzou.

Usajili huo ulikamilika katika siku ya mwisho ya dirisha la usajili nchini Algeria, huku JS Kabylie ikifanikiwa kuipita klabu nyingine zilizokuwa zikimuwania kiungo huyo.

Yanga ilimtaka Mabula

Kabla ya kuibukia Algeria, jina la Mabula lilikuwa gumzo kwenye dirisha la usajili nchini Tanzania baada ya Yanga kuanza mazungumzo ya kumrudisha nyumbani.

Iliripotiwa mwezi Julai kwamba Yanga ilikuwa imeanza mazungumzo na Mabula, ikiwa na lengo la kumuongeza katika eneo la kiungo mkabaji. Wakati huo Mabula alikuwa amemaliza mkataba wake na Shamaxi na alikuwa mchezaji huru.

Baadaye, taarifa zikaeleza kuwa mazungumzo hayo hayakuzaa matunda kutokana na tofauti za kifedha ambapo upande wa Mabula ulihitaji ofa ya uhamisho iliyokadiriwa kufikia karibu Sh1.5 bilioni, pamoja na mshahara wa takribani dola 14,000 kwa mwezi, huku Yanga ikiishia kwenye ofa ya zaidi ya Sh600 milioni ambayo haikukidhi mahitaji ya upande wa mchezaji.

Kabla ya dili la Yanga kufifia, pia Mabula alikuwa akihusishwa na Kasimpasa ya Uturuki, huku taarifa za awali zikidai klabu hiyo ilikuwa ikimfuatilia kwa karibu.


  

More Stories

Keffe D apatikana na hatia ya mauaji ya Tupac Shakur baada ya miaka 30
Keffe D apatikana na hatia ya mauaji ya Tupac Shakur baada ya miaka 30
Today, READ MORE β†’
Agosti Yawaweka Kichwa kwa Kichwa Gueye na Nzengeli kwa Tuzo ya Mchezaji Bora
Agosti Yawaweka Kichwa kwa Kichwa Gueye na Nzengeli kwa Tuzo ya Mchezaji Bora
Today, READ MORE β†’
Mabula aibukia JS Kabylie
Mabula aibukia JS Kabylie
Today, READ MORE β†’
Yanga kuanza kampeni za kimataifa na jezi mpya
Yanga kuanza kampeni za kimataifa na jezi mpya
Today, READ MORE β†’
Waamuzi wanne kutoka Tanzania wateuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika
Waamuzi wanne kutoka Tanzania wateuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika
Today, READ MORE β†’
Waamuzi wa Tanzania kuchezesha JS Saoura dhidi ya Horoya
Waamuzi wa Tanzania kuchezesha JS Saoura dhidi ya Horoya
Today, READ MORE β†’
Uwanja ndio sababu hatufungi magoli mengi : Steve Berker Kocha wa Simba
Uwanja ndio sababu hatufungi magoli mengi : Steve Berker Kocha wa Simba
Today, READ MORE β†’
Mashabiki wa Simba wamgusa Doumbia kwa ujumbe wa upendo
Mashabiki wa Simba wamgusa Doumbia kwa ujumbe wa upendo
Today, READ MORE β†’
Nasreddine Nabi aachana rasmi na Raja Casablanca
Nasreddine Nabi aachana rasmi na Raja Casablanca
Today, READ MORE β†’
Saka Aipa Arsenal Ushindi wa Pili Mfululizo, Clean Sheet Bado Haijavunjwa.
Saka Aipa Arsenal Ushindi wa Pili Mfululizo, Clean Sheet Bado Haijavunjwa.
Today, READ MORE β†’