Mwandishi mashuhuri wa masuala ya usajili duniani, Fabrizio Romano, amezindua rasmi jezi mpya za Young Africans (Yanga SC) ambazo klabu hiyo inatarajiwa kutumia katika kampeni yake ya CAF Champions League msimu wa 2026/27.
Uzinduzi huo umeongeza mvuto kuelekea safari ya Yanga katika mashindano ya kimataifa, huku klabu hiyo ikitarajiwa kuingia kwenye michuano hiyo ikiwa na malengo ya kufanya vizuri na kuiwakilisha Tanzania kwa kiwango cha juu.
Jezi hizo zimepokea attention kubwa kutokana na namna zilivyowasilishwa na jina la Fabrizio Romano, ambaye ni miongoni mwa watu wanaotambulika zaidi duniani katika utoaji wa taarifa za soka. Kwa upande wa Wananchi, ujio wa jezi hizo unaongeza hamasa kuelekea mechi za CAF Champions League.
HERE WE GO — Levels za kimataifa. Yanga sasa inaelekeza nguvu zake kwenye jukwaa la Afrika, huku mashabiki wakisubiri kwa hamu kuona timu yao ikianza rasmi safari ya kuwania mafanikio katika mashindano hayo ya juu ya klabu barani Afrika..jpg)





