Yanga kumtumia Fabrizio romano kutambulisha jezi si jambo jipya

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said • 3rd September 2026


Yanga kumtumia Fabrizio romano kutambulisha jezi si jambo jipya

Mchambuzi wa soka, Salumu Mnolela, amesema hatua ya Yanga SC kutumia mwandishi maarufu wa habari za usajili, Fabrizio Romano, kutambulisha jezi zake mpya za kimataifa za msimu wa 2026/27 si jambo geni katika soka la Tanzania.

Mnolela amesema klabu za Tanzania zimewahi kutumia watu mashuhuri wa kimataifa katika shughuli za utambulisho na uendelezaji wa chapa zao, akitoa mfano wa Simba SC ambayo mwaka 2020 ilihusisha beki wa zamani wa Barcelona na Timu ya Taifa ya Uhispania, Gerard Piqué, katika shughuli iliyohusiana na klabu hiyo.

Amesema matumizi ya majina makubwa ya kimataifa katika masoko na utambulisho wa bidhaa za klabu ni sehemu ya mikakati ya kibiashara inayolenga kuongeza mwonekano na mvuto wa klabu katika soko la kimataifa. Kwa msingi huo, amewataka mashabiki na wadau wa soka kulitazama suala la Yanga kutumia Fabrizio Romano kama sehemu ya ushindani wa kibiashara na ujenzi wa chapa kati ya klabu hiyo na Simba.


  

More Stories

TPLB yasisitiza, mabadiliko ya ratiba hayataathiri mwisho wa ligi
TPLB yasisitiza, mabadiliko ya ratiba hayataathiri mwisho wa ligi
Today, READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 03 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 03 2026
Today, READ MORE →
Al Ahli Tripoli yawasili Zanzibar kwa mtanange wa CAF dhidi ya KMKM.
Al Ahli Tripoli yawasili Zanzibar kwa mtanange wa CAF dhidi ya KMKM.
Today, READ MORE →
Gaborone United Yaitambua Yanga: “Hautakuwa Mchezo Mwepesi”
Gaborone United Yaitambua Yanga: “Hautakuwa Mchezo Mwepesi”
Today, READ MORE →
Kwa Shalulile Simba walianza Yanga wakamaliza, kocha Barker akihusika
Kwa Shalulile Simba walianza Yanga wakamaliza, kocha Barker akihusika
Today, READ MORE →
Yanga kumtumia Fabrizio romano kutambulisha jezi si jambo jipya
Yanga kumtumia Fabrizio romano kutambulisha jezi si jambo jipya
Today, READ MORE →
Fabrizio Romano Azindua Jezi za Yanga kwa Ajili ya CAF Champions League.
Fabrizio Romano Azindua Jezi za Yanga kwa Ajili ya CAF Champions League.
Today, READ MORE →
Simba yatangaza ujio wa Simba marathon kwenye maadhimisho ya miaka 90
Simba yatangaza ujio wa Simba marathon kwenye maadhimisho ya miaka 90
Yesterday, READ MORE →
Uganda U23 yajitoa kwenye mbio za kufuzu AFCON U23 2027
Uganda U23 yajitoa kwenye mbio za kufuzu AFCON U23 2027
Yesterday, READ MORE →
Chelsea yasalitiwa kwa lamine siku ya mwisho ya usajili
Chelsea yasalitiwa kwa lamine siku ya mwisho ya usajili
Yesterday, READ MORE →