Mshambuliaji wa Ghana, Jonathan Sowah, amezungumzia tukio lililowahi kuibua mjadala mkubwa wakati akitambulishwa kama mchezaji wa Simba SC, ambapo alionekana kuchana picha ya Rais wa Yanga SC, Eng. Hersi Said.
Sowah amesema kitendo hicho hakikuwa uamuzi wake binafsi, akieleza kuwa wakati huo hakuwa na namna wala chaguo la kufanya tofauti na alichoelekezwa. Kwa mujibu wa mshambuliaji huyo, alikuja Tanzania akiwa na lengo la kutafuta maisha na kipato kupitia soka.
“Kuna wakati huwa najisikia vibaya, kile kilichotokea sikuwa na namna wala sikuwa na chaguo lolote. Nilikuja huku kutafuta pesa, nilipaswa kufanya kile wanachotaka nifanye.”
Kauli hiyo imefungua mjadala mpya kuhusu tukio hilo, huku Sowah akisisitiza kuwa hakuchukua hatua hiyo kwa hiari yake. Tukio hilo lilitokea katika mazingira ya utambulisho wake Simba na baadaye likawa miongoni mwa matukio yaliyokumbukwa na mashabiki wa soka nchini.
Kwa sasa Sowah anaendelea na safari yake ya soka akiwa na Singida Black Stars, baada ya kuondoka Simba SC, huku akitazamia kuacha matukio ya nje ya uwanja na kuendelea kujenga jina lake kupitia uwezo wake ndani ya uwanja.



