Kiungo mshambuliaji wa FC Dallas ya Marekani, Bernard Kamungo, mwenye umri wa miaka 24, ameitwa rasmi kwenye kikosi cha Taifa Stars kwa ajili ya michezo ya kufuzu AFCON 2027.
Kamungo anarejea kuipa kipaumbele Tanzania katika ngazi ya kimataifa baada ya hapo awali kuitumikia Marekani katika kikosi cha U-23, pamoja na kucheza mchezo mmoja wa kirafiki akiwa na kikosi cha Senior Team.
Kuitwa kwake Taifa Stars kunatarajiwa kuongeza ubunifu na nguvu katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo, huku mashabiki wakisubiri kumuona akivaa jezi ya Tanzania katika michezo ijayo ya kimataifa.



