Bodi ya ligi tanzania bara yafuta kadi nyekundu ya Gibril sillah wa Azam

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said β€’ 4th September 2026


Bodi ya ligi tanzania bara yafuta kadi nyekundu ya Gibril sillah wa Azam

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi Kuu imefuta rasmi adhabu ya kadi nyekundu aliyopewa mchezaji wa Azam FC, Gibril Sillah, katika mchezo namba 034 dhidi ya Kagera Sugar uliomalizika kwa Azam FC kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya kamati kupitia picha jongeo pamoja na taarifa za wataalamu na kujiridhisha kuwa Sillah hakustahili kupewa kadi hiyo. Kamati imesema uamuzi huo umezingatia Kanuni ya 12:8 ya Ligi Kuu inayohusu Usimamizi wa Ligi.

Wakati huo huo, kamati imempa onyo kali mwamuzi wa akiba wa mchezo huo, Greyson Buchard kutoka Kagera, kwa kile ilichokieleza kuwa ni mapungufu ya kiuchezeshaji yaliyotokana na kushindwa kutafsiri ipasavyo sheria za mchezo. Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 43:1(1.8) inayohusu Udhibiti kwa Waamuzi.


  

More Stories

Massanza akumbana na fainali kamati ya saa 72
Massanza akumbana na fainali kamati ya saa 72
Today, READ MORE β†’
Kangwanda: Tumejiandaa vizuri, tutatoa kila kitu uwanjani.
Kangwanda: Tumejiandaa vizuri, tutatoa kila kitu uwanjani.
Today, READ MORE β†’
Bodi ya ligi tanzania bara yafuta kadi nyekundu ya Gibril sillah wa Azam
Bodi ya ligi tanzania bara yafuta kadi nyekundu ya Gibril sillah wa Azam
Today, READ MORE β†’
Mngqithi: Gaborone United ni timu imara, Yanga inakabiliwa na mtihani mgumu.
Mngqithi: Gaborone United ni timu imara, Yanga inakabiliwa na mtihani mgumu.
Today, READ MORE β†’
Ahmed Ally atuma ujumbe mzito kwa wachezaji wa Simba kuelekea mchezo dhidi ya Mighty wanderers
Ahmed Ally atuma ujumbe mzito kwa wachezaji wa Simba kuelekea mchezo dhidi ya Mighty wanderers
Today, READ MORE β†’
Aziz KI apewa mazoezi ya ziada kuingamiza Gaborone united kesho
Aziz KI apewa mazoezi ya ziada kuingamiza Gaborone united kesho
Today, READ MORE β†’
Bernard Kamungo ajumuishwa rasmi kwenye kikosi cha Taifa Stars.
Bernard Kamungo ajumuishwa rasmi kwenye kikosi cha Taifa Stars.
Today, READ MORE β†’
Kikosi Cha awali Taifa Stars hadharani kufuzu Afcon 2027
Kikosi Cha awali Taifa Stars hadharani kufuzu Afcon 2027
Today, READ MORE β†’
CAF yakagua arusha kujiweka tayari kwa afcon 2027.
CAF yakagua arusha kujiweka tayari kwa afcon 2027.
Today, READ MORE β†’
Rushine aahidi makubwa kimataifa, Simba ikielekea malawi
Rushine aahidi makubwa kimataifa, Simba ikielekea malawi
Today, READ MORE β†’