Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Miguel Gamondi, ameongozana na maafisa wa benchi la ufundi pamoja na viongozi wa TFF katika ziara ya Simba SC, ikiwa ni sehemu ya kujenga na kuimarisha ushirikiano kati ya klabu hiyo na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), hususan katika masuala yanayohusu Timu za Taifa.
Ziara hiyo inalenga kuimarisha mawasiliano na mahusiano kati ya Simba na TFF, ili pande hizo ziweze kufanya kazi kwa pamoja kwa manufaa ya Taifa Stars.
Gamondi ndiye Kocha Mkuu wa Taifa Stars, huku TFF ikiendelea kumshirikisha pamoja na benchi lake la ufundi katika mipango na maandalizi ya timu ya taifa.