Local, Transfer News, TRA United

Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1h ago
Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige

Klabu ya TRA United inatajwa kumteua kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Hemed Suleiman (56), kuwa kocha mpya wa timu hiyo, akichukua nafasi ya Etienne Ndayiragije ambaye alitimuliwa siku chache zilizopita.

Hemed anarejea kwenye soka la ushindani akiwa na jukumu la kuiongoza TRA United katika kipindi ambacho timu hiyo inatafuta mwendelezo mzuri wa matokeo.

Ujio wa Hemed unafuatia taarifa za awali zilizohusisha TRA United na kocha wa zamani wa Mbeya City, Meckie Mexime, ambaye inadaiwa alisimamia mazoezi ya timu hiyo siku ya Jumanne wakati klabu ikiwa katika mchakato wa kumpata kocha mpya.

Hata hivyo, TRA United imeamua kumpa nafasi Hemed, ambaye ana uzoefu mkubwa katika soka la Tanzania, ikiwemo kipindi alichokuwa sehemu ya benchi la ufundi la Taifa Stars.

Kocha huyo sasa anakabiliwa na jukumu la kuijenga upya TRA United na kuhakikisha timu hiyo inapata matokeo yatakayoiweka kwenye nafasi nzuri baada ya kuanza kwa kuchechea katika msimu huu.

More Stories

Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
40m ago
READ MORE β†’
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea
1h ago
READ MORE β†’
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
1h ago
READ MORE β†’
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
3h ago
READ MORE β†’
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
3h ago
READ MORE β†’
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
3h ago
READ MORE β†’
NBC PREMIER LEAGUE: Mashujaa na Singida Bs kuingia kwenye vita ya kusaka alama tatu.
NBC PREMIER LEAGUE: Mashujaa na Singida Bs kuingia kwenye vita ya kusaka alama tatu.
3h ago
READ MORE β†’
Mafanikio ya Yanga hayajaanza leo, yalianza kwa maono ya wazee
Mafanikio ya Yanga hayajaanza leo, yalianza kwa maono ya wazee
4h ago
READ MORE β†’
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: matokeo ya usiku huu.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: matokeo ya usiku huu.
14h ago
READ MORE β†’