Local, Normal News, Simba Sc

Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1h ago
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea

Mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Doumbia, amekiri kuwa anapitia kipindi kigumu cha kutofunga mabao katika hatua za mwanzo za msimu, akisema hali hiyo ni jambo jipya kwake tangu aanze kucheza soka la ushindani.

Doumbia amesema licha ya kupata nafasi za kucheza, bado hajafanikiwa kufungua akaunti yake ya mabao, hali ambayo amesema haijawahi kumkuta katika hatua kama hii ya msimu.

“Ni mara ya kwanza kabisa kwangu kupitia kipindi cha aina hii, kwa sababu hii ni ligi ambayo ndiyo kwanza imeanza. Kwa hiyo ni jambo la kawaida, hasa unapokuwa unapata nafasi yako ya kwanza. Hivyo, hii ni mara yangu ya kwanza kupitia hali kama hii,” amesema Doumbia.

Hata hivyo, mshambuliaji huyo anaendelea kupata sapoti kutoka kwa mashabiki wa Simba, huku benchi la ufundi chini ya kocha Steve Barker likionyesha imani kwake licha ya changamoto hiyo ya kufunga.

Doumbia pia ameendelea kuonyesha dalili za uwezo wake kila anapopewa nafasi. Katika dakika chache alizocheza kwenye mchezo uliopita dhidi ya Mighty Wanderers, mshambuliaji huyo alionyesha ubora na uwezo wa kuleta tofauti katika safu ya ushambuliaji.

Kwa sasa, kinachosubiriwa ni Doumbia kupata bao lake la kwanza, ambalo linaweza kuwa mwanzo wa kuondoa presha na kumfungulia njia ya kurejea kwenye kiwango ambacho mashabiki wa Simba wanakitarajia kutoka kwake.

More Stories

Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
38m ago
READ MORE β†’
Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige
Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige
1h ago
READ MORE β†’
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
1h ago
READ MORE β†’
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
3h ago
READ MORE β†’
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
3h ago
READ MORE β†’
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
3h ago
READ MORE β†’
NBC PREMIER LEAGUE: Mashujaa na Singida Bs kuingia kwenye vita ya kusaka alama tatu.
NBC PREMIER LEAGUE: Mashujaa na Singida Bs kuingia kwenye vita ya kusaka alama tatu.
3h ago
READ MORE β†’
Mafanikio ya Yanga hayajaanza leo, yalianza kwa maono ya wazee
Mafanikio ya Yanga hayajaanza leo, yalianza kwa maono ya wazee
4h ago
READ MORE β†’
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: matokeo ya usiku huu.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE: matokeo ya usiku huu.
14h ago
READ MORE β†’