Local, Normal News, Singida BS, Mashujaa FC

Kimoto akalia kuti kavu baada ya kipigo dhidi ya Mashujaa Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2h ago
Kimoto akalia kuti kavu baada ya kipigo dhidi ya Mashujaa Fc

Mustakabali wa Kocha Mkuu wa Singida Black Stars, Papy Kimoto, ndani ya kikosi hicho unadaiwa kuwa shakani, huku kukiwa na ripoti kuwa uongozi wa klabu hiyo unafikiria kumfuta kazi kufuatia kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma leo.

Habari kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa, mbali na matokeo hayo mabaya ya uwanjani, hakuna maelewano mazuri kati ya kocha huyo raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na mabosi wake.

Chanzo cha kuaminika kimebainisha kuwa mgogoro huo ulisababishwa na hitaji la Kocha Kimoto kutaka wachezaji wote waliosafiri kwenda Sudan Kusini kwa ajili ya michuano ya CAF kuelekea moja kwa moja Kigoma.

Hata hivyo, uongozi ulikataa mpango huo kwa sababu za kiuchumi na kiwepesi, na badala yake ukaagiza wachezaji 12 pekee wasafiri kwa ndege kuungana na kikosi kilichokuwa kimebaki Singida, jambo ambalo linatajwa kumkasirisha kocha huyo.

More Stories

Clara Luvanga aweka historia Marekani, asajiliwa kwa rekodi Tanzania
Clara Luvanga aweka historia Marekani, asajiliwa kwa rekodi Tanzania
2h ago
READ MORE β†’
Gamondi ateta na viongozi, benchi la ufundi Yanga
Gamondi ateta na viongozi, benchi la ufundi Yanga
2h ago
READ MORE β†’
Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
Chama aweka wazi kinachoendelea nje ya uwanja, si sehemu ya maisha yangu
7h ago
READ MORE β†’
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea
7h ago
READ MORE β†’
Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige
Morocco apindua meza TRA United, kumrithi Ndayirajige
8h ago
READ MORE β†’
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
UEFA Champions League kuendelea leo kwa mechi sita za kibabe.
8h ago
READ MORE β†’
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
Mecky mexime kutua TRA, Kuchukua mikoba ya Ndayiragije
9h ago
READ MORE β†’
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
Breaking news: Yanga yataja gharama za ujenzi, Azania bank ikihusika
10h ago
READ MORE β†’
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
Yanga yaanza safari mpya ya ujenzi, ghorofa 12 kujengwa mafia na nyamwezi
10h ago
READ MORE β†’