TRA United imemtangaza rasmi Hemed Suleiman “Morocco” kuwa kocha Mkuu wa timu hiyo, akichukua nafasi ya Etienne Ndayiragije ambaye ametenguliwa na klabu hiyo.
Morocco anarudi kwenye benchi la TRA United akiwa na jukumu la kurekebisha mwenendo wa timu na kuhakikisha inapata matokeo mazuri katika michezo ijayo ya NBC Premier League.
Uongozi wa TRA United sasa unaweka imani kwa kocha huyo mpya kuiongoza timu katika hatua inayofuata, huku mashabiki wakisubiri kuona mabadiliko yatakayofanywa na Morocco ndani ya kikosi.