CAF Champions League inaendelea leo jijini Dar es Salaam, ambapo Simba SC itashuka Uwanja wa Uhuru kuikabili Mighty Wanderers ya Malawi katika mchezo wa marudiano wa hatua ya awali.
Simba inaingia kwenye mchezo huu ikiwa na faida ya bao 1-0 iliyopatikana katika mchezo wa kwanza nchini Malawi kupitia bao la Anicet Oura.
Wekundu wa Msimbazi wanahitaji kulinda faida hiyo na kuhakikisha wanafuzu kwenda hatua inayofuata ya michuano hiyo ya juu Afrika.
Mighty Wanderers, kwa upande wao, wanahitaji ushindi ili kubadilisha matokeo ya jumla na kuendelea na safari yao katika CAF Champions League.
Mchezo huo unapigwa leo Uwanja wa Uhuru kuanzia saa 10:00 jioni.