Local, Transfer News, Power Dynamos, Yanga, Sekhukhune United

Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1h ago
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia

Mshambuliaji wa DR Congo, Andy Bobwa Boyeli, ameibukia nchini Zambia baada ya kujiunga rasmi na klabu ya Power Dynamos, inayoshiriki Ligi Kuu ya Zambia.

Boyeli amesaini mkataba wa miaka miwili na nusu na mabingwa hao wa ligi kuu ya Zambia, akianza ukurasa mpya wa maisha yake ya soka baada ya kuachana na klabu ya Sekhukhune United ya Afrika Kusini.

Mshambuliaji huyo mwenye asili ya DR Congo amejiunga na Power Dynamos akiwa mchezaji huru, baada ya kumaliza mkataba wake na Sekhukhune United.

Boyeli si mgeni katika soka la Afrika Mashariki, baada ya kuwahi kuvaa jezi ya Young Africans (Yanga SC) ya Tanzania, kabla ya kuendelea na safari yake ya soka katika ligi ya Afrika Kusini.

Aliitumikia Yanga msimu uliopita kwa mkopo ambao hata hivyo ulisitishwa baada ya miezi sita tu baada ya Wananchi kutoridhishwa na kiwango chake.

Amerejea tena Power Dynamos klabu iliyomtambulisha awali na kumpa nafasi ya kusajiliwa na Sekhukhune United.

More Stories

Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
11m ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
11m ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
53m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
1h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
9h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
13h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
14h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
16h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
16h ago
READ MORE β†’