Licha ya mashabiki wa Yanga kutamani kumuona kiungo mshambuliaji Stephane Aziz Ki pengine akianza kila mchezo, Kocha Mkuu wa Yanga Manqoba Mngqithi amesisitiza kuwa nyota huyo bado hajafikia utimamu wa mwili wa asilimia 100 kuweza kucheza dakika 90.
Kwenye mchezo uliopita wa hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Gaborone United, Aziz Ki alitumika kwa dakika 45 za kipindi cha pili huku akiwekwa kwenye ulinzi mkali na wachezaji wa Gaborone ambao walihakikisha wanakuwa wengi kumdhibiti kila alipogusa mpira.
Manqoba amesisitiza kuwa Aziz Ki ataendelea kucheza dakika 45 hadi 60 kwa wakati huu ambao anaendelea kuimarika huku akisisitiza kuwa nyota huyo ni mchezaji muhimu katika mipango ya Yanga hasa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa (CAFCL).
"Kwa sasa fitness yake imeongezeka tofauti na alipojiunga nasi, nitaendelea kumpa dakika za kucheza ili awe timamu zaidi. Bado sifikirii kumpa zaidi ya dakika 60 kwani bado hajafikia kwenye kiwango cha utimamu anachopaswa kuwa. "
"Aziz Ki ni mtu muhimu sana kiufundi na ataongeza thamani kubwa kwenye kikosi chetu pale atakapokuwa fit kwa asilimia 100," alisema Manqoba
Baada ya kutoanza mchezo uliopita, kuna uwezekano mkubwa Manqoba akamuanzisha Aziz Ki kesho kwenye mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa dhidi ya Gaborone United