Baada ya kufanikiwa kutinga raundi ya kwanza ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-2 dhidi ya Gaborone United, kikosi cha Yanga sasa kinarejesha makali yake kwenye ligi kuu ya NBC.
Kesho Jumanne, saa 1 usiku, Yanga itashuka dimba la KMC Complex kuwakabili Geita Gold katika mchezo wa raundi ya 6.
Vinara hao wa ligi kuu, watashuka dimbani wakiwa na dhamira ya kuendeleza makali yao waliyoanza nayo msimu huu.
Yanga inaongoza ligi ikikusanya alama 15 baada ya mechi tano, ushindi dhidi ya Geita Gold utawahakikishia Wananchi kuendelea kusalia katika nafasi hiyo.
Huo utakuwa mchezo wa mwisho wa ligi mwezi huu kabla ya kalenda ya FIFA. Mchezo utakaofuata ni dhidi ya Simba Oktoba 10